And before this ˹Quran˺ the Book of Moses was ˹revealed as˺ a guide and mercy. And this Book is a confirmation, in the Arabic tongue, to warn those who do wrong, and as good news to those who do good.
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qira'at
Hadith
Na kabla ya hii Qur’ani, tuliiteremsha Taurati ikiwa ni muongozo kwa Wana wa Isrāīl waiandame na ni rehema kwa wenye kuiamini na kuifuata kivitendo. Na hii Qur’ani inasadikisha Vitabu vilivyokuwa kabla yake. Tumeiteremsha kwa lugha ya Kiarabu ili iwaonye wale waliozidhulumu nafsi zao kwa kukanusha na kuasi. Na bishara njema ni ya wale waliomtii Mwenyezi Mungu na wakafanya wema katika Imani yao na utiifu wao duniani.