Sign in
Sign in
Sign in
Select Language

Tafsir: Al-Anfal 8:24

8:24
يا ايها الذين امنوا استجيبوا لله وللرسول اذا دعاكم لما يحييكم واعلموا ان الله يحول بين المرء وقلبه وانه اليه تحشرون ٢٤
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ ٱسْتَجِيبُوا۟ لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ ۖ وَٱعْلَمُوٓا۟ أَنَّ ٱللَّهَ يَحُولُ بَيْنَ ٱلْمَرْءِ وَقَلْبِهِۦ وَأَنَّهُۥٓ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ ٢٤
يَٰٓأَيُّهَا
ٱلَّذِينَ
ءَامَنُواْ
ٱسۡتَجِيبُواْ
لِلَّهِ
وَلِلرَّسُولِ
إِذَا
دَعَاكُمۡ
لِمَا
يُحۡيِيكُمۡۖ
وَٱعۡلَمُوٓاْ
أَنَّ
ٱللَّهَ
يَحُولُ
بَيۡنَ
ٱلۡمَرۡءِ
وَقَلۡبِهِۦ
وَأَنَّهُۥٓ
إِلَيۡهِ
تُحۡشَرُونَ
٢٤
O believers! Respond to Allah and His Messenger when he calls you to that which gives you life. And know that Allah stands between a person and their heart, and that to Him you will all be gathered.
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qira'at
Hadith
Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu kuwa ni Mola na Muhammad kuwa ni Nabii na ni Mtume, Itikieni mwito wa Mwenyezi Mungu na wa Mtume kwa kumtii awaitapo kwenye haki yenye kuwapa uhai. Kwani katika kuitikia mwito huo kunatengeneza maisha yenu katika ulimwengu na Akhera. Na mjue, enyi Waumini, kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Mwenye kuendesha kila kitu na Ndiye Muweza, Anaingilia kati baina ya mtu na kile ambacho moyo wake unakitamani. Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayestahiki kuitikiwa Akiwaita, kwani mamlaka ya kila kitu yako mkononi Mwake. Na jueni kwamba nyinyi mtakusanywa kwa Siku isiyo na shaka, ambapo kila mmoja atalipwa kwa analostahili kulipwa.