˹Remember˺ when the angels proclaimed, “O Mary! Allah gives you good news of a Word1 from Him, his name will be the Messiah,2 Jesus, son of Mary; honoured in this world and the Hereafter, and he will be one of those nearest ˹to Allah˺.
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qira'at
Hadith
Kadhalika hukuwako huko, ewe Nabii wa Mwenyezi Mungu, pindi Malaika waliposema, «Ewe Maryam, Mwenyezi Mungu Anakubashiria mtoto ambaye kupatikana kwake kutatokana na neno la Mwenyezi Mungu, yaani Atamwambia, ‘Kuwa,’ na atakuwa, jina lake ni Al-Masīḥ ‘Īsā mwana wa Maryam. Yeye atakuwa na jaha katika ulimwengu na Akhera na atakuwa ni miongoni mwa wenye kukurubishwa kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.