هؤلاء المتواضعون الخاشعون مِن صفاتهم أنهم إذا ذُكِر الله وحده خافوا عقابه، وحَذِروا مخالفته، وإذا أصابهم بأس وشدة صبروا على ذلك مؤملين الثواب من الله عز وجل، وأدَّوْا الصلاة تامة، وهم مع ذلك ينفقون مما رزقهم الله في الواجب عليهم مِن زكاة ونفقة عيال، ومَن وَجَبَتْ عليهم نفقته، وفي سبيل الله، والنفقات المستحبة.
تفاسير
الطبقات
فوائد
تدبرات
الإجابات
قراءات
الحديث
Wanyenyekevu hawa wenye kujinyongesha (kwa Mwenyezi Mungu) miongoni mwa sifa zao ni kwamba wao Atajwapo Mwenyezi Mungu Peke Yake, wanaiyogopa adhabu Yake na wanakuwa na hadhari wasimuasi, na wakipatikana na shida na matatizo, wanasubiri juu ya hayo wakiwa na matumaini kupata malipo mema kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, wanatekeleza Swala kikamilifu, na wao pamoja na hayo wanatoa, katika kile Alichowaruzuku Mwenyezi Mungu, katika mambo yanayowapasa ya Zaka, matumizi ya watoto na kila ambaye matumizi yake yanawalazimu, katika njia ya Mwenyezi Mungu na katika matumizi yanayopendekezwa yasio ya lazima.