مثل فريقَي الكفر والإيمان كمثل الأعمى الذي لا يرى والأصم الذي لا يسمع والبصير والسميع: ففريق الكفر لا يبصر الحق فيتبعه، ولا يسمع داعي الله فيهتدي به، أما فريق الإيمان فقد أبصر حجج الله وسمع داعي الله فأجابه، هل يستوي هذان الفريقان؟ أفلا تعتبرون وتتفكرون؟
تفاسير
الطبقات
فوائد
تدبرات
الإجابات
قراءات
الحديث
Mfano wa makundi mawili, ya ukafiri na Imani, ni mfano wa kipofu asiyeona na kiziwi asiyesikia na yule anayeona na kusikia: kundi la ukafiri haliioni haki likapata kuifuata wala halimsikii mlinganizi wa Mwenyezi Mungu likapata kuongoka kwa sababu yake. Ama kundi la Imani limishaziona hoja za Mwenyezi Mungu na limemsikia mlinganizi wa Mwenyezi Mungu na limemuitikia. Je, yanafanana makundi mawili haya? Kwani hamzingatii na mkafikiri?