And those who were mindful of their Lord will be led to Paradise in ˹successive˺ groups. When they arrive at its ˹already˺ open gates, its keepers will say, “Peace be upon you! You have done well, so come in, to stay forever.”
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qira'at
Hadith
Na wataongozwa wale waliomcha Mola wao, kwa kumpwekwsha na kufanya vitendo vya utiifu Kwake, wapelekwe Peponi, makundi kwa makundi. Na watakapoifikia na waombewe kuingia, milango yake itafunguliwa, na Malaika waliowakilishwa kuisimamia Pepo watawakongowea na watawaamkia kwa ucheshi na furaha kwa kuwa wamesafishika na athari za maasia na watawaambia, «Amani iwe juu yenu! Mmesalimika na kila baya. Hali zenu ni nzuri. Basi ingieni Peponi mkae milele humo.»