این است [فرمان الله]، و هر کس دستورهای دینی و الهی را بزرگ بشمارد، یقیناً این [بزرگداشت، نشانهای] از پرهیزگاری دلهاست.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Hayo ndiyo Aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu ya kumpwekesha na kumtakasia ibada. Na yoyote mwenye kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu na akayatukuza mambo makubwa ya Dini, na miongoni mwayo ni matendo ya Hija na sehemu zake na wanyama wanaochinjwa huko, kwa kuchagua walio wazuri na walio wanono, basi kutukuza huko ni katika vitendo vya wenye nyoyo zenye kusifika kwa kumcha Mwenyezi Mungu na kumuogopa.