آیا نمیدانی که فرمانرواییِ آسمانها و زمین از آنِ الله است و شما جز الله [هیچ] دوست و یاوری ندارید [که کارسازتان باشد]؟
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Kwani hukujua, ewe Nabii, wewe na ummah wako, kwamba Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ndiye Mwenye kumiliki, Ndiye Mwenye kuendesha mambo ya mbinguni na ardhini? Anafanya Analolitaka na Anatoa uamuzi Anaotaka. Anawaamrisha waja Wake na kuwakataza Anavyotaka, na ni juu yao kutii na kukubali. Na wajue wenye kumuasi Yeye kuwa hakuna rafiki mwenye kuwasaidia wala muokozi mwenye kuzuia adhabu ya Mwenyezi Mungu isiwapate.