و اینچنین نشانهها [و دلایل قدرت الهی] را گوناگون بیان میکنیم تا مبادا [مشرکان] بگویند: «[آنها را از اهل کتاب] آموختهای»؛ و ما آنها را برای گروهی که میدانند [و میفهمند] به روشنی بیان میکنیم.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Na kama tulivyowafafanulia washirikina, katika hii Qur’ani, hoja zilizo wazi juu ya jambo la kumpwekesha Mwenyezi Mungu, utume na marejeo ya Kiyama, tunawafafanulia hoja katika kila wasichokijua. Na hapo wanasema urongo, «Umejifunza kutoka kwa watu wa Kitabu!» Na ili tufafanue haki, kwa kuzileta aya, kwa watu wanaoijua na kuikubali na kuifuata, nao ni waliomuamini Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kile alichoteremshiwa.