[پیام الهی را در حالی میشنوند که] دلهایشان غافل است؛ و کسانی که [کافر و] ستمکار بودند، نجواهایشان را پنهان کردند [و گفتند:] «آیا این [مدعى پیامبرى،] جز بشرى همچون شماست؟ آیا در حالی که [حقیقت را] میبینید، به جادو روی میآورید؟»
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Nyoyo zao zimeghafilika na Qur’ani, zimeshughulika na ubatilifu wa dunia na matamanio yake, hawayafahamu yaliyomo ndani yake. Lakini madhalimu miongoni mwa Makureshi wamejikusanya pamoja juu ya jambo lililofichika, nalo ni kueneza yale ambayo kwayo wanawazuia watu kumuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa kuwa yeye ni binadamu mfano wao, hatafautiani na wao katika kitu chochote, na kwamba Qur’ani aliyoileta ni uchawi. (Wanawaambia kwa kusema) «Vipi mutakuja kwake na mumfuate na hali kwamba mnaona kwamba yeye ni binadamu kama nyinyi?»