[ای پیامبر،] به کسانی که کفر ورزیدند بگو [که] اگر [از شرک و دشمنی] دست بردارند، گذشتههایشان بخشوده میشود و[لی] اگر [به رفتار گذشتۀ خود] بازگردند، سنت [و عذاب الهى كه در مورد] پیشینیان گذشت [تكرار خواهد شد].
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wale waliokanusha upweke wa Mwenyezi Mungu miongoni mwa Washirikina wa watu wako kwamba watakomeka na ukafiri na kumfanyia uadui Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, na wakarudi kumuamini Mwenyezi Mungu Peke Yake na kutompiga vita Mtume na Waumini, Mwenyezi Mungu Atawasamehe madhambi yaliyopita, kwani Uislamu unafuta yaliyopita. Na watakaporudia washirikina hawa kukupiga vita baada ya tukio ambalo ulipata ushindi juu yao siku ya Badr, basi mwendo wa watu wa mwanzo umetangulia, nao ni kwamba wao wakikanusha na wakaendelea kwenye ukaidi wao, tutawaletea adhabu na mateso kwa haraka.