پس [صالح] از آنان روی گردانْد و گفت: «ای قوم من، من پیام پروردگارم را به شما رساندم و برایتان خیرخواهی کردم؛ ولى شما [خیرخواهان و] نصیحتگران را دوست ندارید».
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Ṣāliḥ, amani imshukie, alijiepusha na watu wake, walipomchinja ngamia, na maangamivu yakawa ni yenye kuwashukia, na akasema kuwaambia, «Enyi watu wangu! Nimewafikishia yale Mola wangu Aliyoniamuru niwafikishie, kuhusu maamrisho Yake na makatazo Yake, na nimewafanyia bidii kiasi nilichoweza katika kuwavutia kwenye kheri na kuwakemea shari na kuwa muaminifu, lakini nyinyi hamuwapendi waaminifu kwenu, ndipo mkayakataa maneno yao na mkamtii kila shetani aliyelaaniwa.»