چگونه [یگانگیِ] الله را انکار میکنید در حالى كه وجودی نداشتید و او به شما زندگی بخشید؛ سپس شما را دستخوش مرگ مىگردانَد و دوباره زنده خواهد كرد؛ آنگاه [برای حساب و جزا] به پیشگاهش بازگردانده مىشوید؟
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Vipi mtaukanusha, enyi washirikina, umoja wa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na kumshirikisha mwengine katika Ibada, pamoja na kuwa kuna dalili zisizopingika kuhusu hilo katika nafsi zenu? Mlikuwa hamko, hamjaumbwa, Akawafanya muweko kwa kuwaumba, Akapuliza kwenu uhai, kisha Atawafisha baada ya kumalizika muda wenu wa kuishi Aliowaekea, kisha Atawarudisha mkiwa na uhai Siku ya Kufufuliwa, kisha mtarejeshwa Kwake mhesabiwe na mlipwe.