همان كسانى كه بخل مىورزند و مردم را به بخل وامیدارند؛ و هر کس [از انفاق] روى بگرداندَ، [بداند كه] الله بىنیازِ ستوده است.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Hawa wenye kujiona ndio wale wanaoyafanyia ubahili mali yao, wasiyatoe katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wakawaamuru watu wawe mabahili kwa kuwapambia huo ubahili. Na yoyote anayezunguka nyuma kwa kuacha kumtii Mwenyezi mungu hamdhuru yoyote isipokuwa nafsi yake, na hatamdhuru Mwenyezi Mungu chochote, kwani Mwenyezi Mungu Ndiye Mkwasi Asiyehitajia viumbe vyake, Mwenye kuhimidiwa Ambaye Ana kila sifa njema iliyokamilika na kila tendo zuri ambalo Anastahiki kushukuriwa kwalo.