برای هر امتی آیینی مقرر کردهایم كه به آن عمل كنند؛ پس [ای پیامبر، پیروان سایر ادیان] نباید با تو در این امر ستیز کنند. به راه پروردگارت دعوت كن؛ [چرا که] تو یقیناً بر [آیینی درست و] راهی راست قرار دارى.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Kila watu miongoni mwa jinsi za watu waliopita tumewaekea sheria na ibada tuliowaamrisha wao kwazo, na wao ni wenye kuzitumia, basi wasikufanyie ushindani, ewe Mtume, hao washirikina wa Kikureshi kuhusu Sheria yako na yale Aliyokuamrisha Mwenyezi Mungu katika matendo ya Hija na aina zote za ibada. Na ulinganie kwenye kumpwekesha Mola wako na kumtakasia ibada na kufuata amri Yake. Hakika wewe uko kwenye Dini iliyolingana sawa, isiyokuwa na mapindi.