اما کسانی که دانش [حقیقی] یافته بودند، گفتند: «وای بر شما! برای کسی که ایمان آورده است و کارهای شایسته میکند، ثواب الهی بهتر است؛ و این [سخن] را کسانی جز شکیبایان نمیپذیرند».
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Na wakasema, wale waliopewa elimu ya kumjua Mwenyezi Mungu na Sheria Yake na wakijua uhakika wa mambo, kuwaambia wale waliosema, «Tunatamani tuwe na mfano wa kile alichopatiwa Qārūn», «Ole wenu! Muogopeni Mwenyezi Mungu na mumtii. Malipo mema ya Mwenyezi Mungu ni bora, kwa aliyemuamini Yeye na Mitume Wake na akafanya matendo mema, kuliko kile alichopatiwa Qārūn. Na haupokei ushauri huu na akaafikiwa kuufuata na kuufanyia kazi isipokua yule anayepigana jihadi na nafsi yake, anayevumilia katika kumtii Mola wake na anayejiepusha na mambo ya kumuasi.