و کسانی كه اگر فرزندان ناتوانى از خود بر جاى بگذارند، بر [آیندۀ] آنان بیم دارند، باید [از ستم دربارۀ یتیمان مردم نیز] بترسند؛ پس باید از الله پروا کنند و سخنی [سنجیده و] درست بگویند.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Na waogope wale ambao lau watakufa na wataacha nyuma yao watoto wadogo madhaifu, wakawachelea dhuluma na kupotea, basi na wamchunge Mwenyezi Mungu juu ya wale mayatima na wengineo walio chini ya mikono yao. Nako ni kuwahifadhia mali yao, kuwalea vizuri na kuwaondolea ya kuwaudhi. Na wawaambie maneno yanayolingana na usawa na wema.