از اموال آنان [= توبهکاران] صدقه [و زکات] بگیر، تا به وسیله آن، آنان را [از گناه] پاک گردانی و درجاتشان را بالا ببری؛ و برایشان دعا کن [چرا که] یقیناً دعای تو [رحمتی برایشان و] مایه آرامش برای آنان است؛ و الله شنوای داناست.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Chukua, ewe Mtume, kwenye mali za hawa waliotubia, waliochanganya matendo mema na matendo mengine maovu, sadaka itakayowasafisha wao na uchafu wa madhambi yao na itakayowainua wao na kuwaondoa kwenye daraja za wanafiki kuwapeleka kwenye daraja za wenye ikhlasi; na watakie wao msamaha wa madhambi yao na uwaombee sitara ya hayo, kwani maombi yako na utakaji msamaha wako ni rehema na utulivu kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Msikizi wa kila maombi na kila neno, ni Mjuzi wa hali za waja Wake na nia zao, na Atamlipa kila mwenye kutenda kwa matendo aliyoyatenda.