و همان ذاتی كه باران را از آسمان به مقدار معینى فرستاد؛ آنگاه سرزمین خزانزده و خشک را به وسیلۀ آن حیات بخشیدیم؛ شما نیز همین گونه [از گورها] بیرون آورده مىشوید.
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Na Aliyeteremsha kutoka mawinguni mvua kwa kipimo, Asiifanye mafuriko yenye kuzamisha wala pungufu isiyotosheleza haja, ipate kuendesha maisha yenu na yale ya wanyama wenu, tukahuisha kwa maji hayo sehemu kubwa ya ardhi kavu isiyokuwa na mimea. Na kama tulivyotoa kwa maji hayo tuliyoyateremsha kutoka juu, kwenye ardhi hiyo iliyokufa, mimea na mazao, hivo ndivyo mtakavyotolewa, enyi watu, makaburini mwenu baada ya kutoweka kwenu.