مَثَل این دو گروه [کافر و مؤمن]، همانند نابینا و ناشنوا [از یک سو] و بینا و شنوا [از سوی دیگر] است. آیا با یکدیگر برابرند؟ آیا پند نمیگیرید؟
تفاسیر
لایهها
درس ها
بازتاب ها
پاسخها
قیراط
حدیث
Mfano wa makundi mawili, ya ukafiri na Imani, ni mfano wa kipofu asiyeona na kiziwi asiyesikia na yule anayeona na kusikia: kundi la ukafiri haliioni haki likapata kuifuata wala halimsikii mlinganizi wa Mwenyezi Mungu likapata kuongoka kwa sababu yake. Ama kundi la Imani limishaziona hoja za Mwenyezi Mungu na limemsikia mlinganizi wa Mwenyezi Mungu na limemuitikia. Je, yanafanana makundi mawili haya? Kwani hamzingatii na mkafikiri?