ceux qui disent, quand un malheur les atteint: "Certes nous sommes à Allah, et c’est à Lui que nous retournerons."
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Miongoni mwa sifa za hawa wenye kusubiri ni kwamba wao wanapofikwa na kitu wanachokichukia husema, «Sisi ni waja waliomilikiwa na Mwenyezi Mungu, tunaoendeshwa kwa amri Yake na mapitisho Yake. Anafanya kwetu Alitakalo. Na sisi Kwake, Peke Yake, ni wenye kurudi kwa kufa, kisha kwa kufufuliwa ili kuhesabiwa na kulipwa.