Ce jour-là, ceux qui n’auront pas cru et auront désobéi au Messager, préféreront que la terre soit nivelée sur eux et ils ne sauront cacher à Allah aucune parole.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Siku litakapokuwa hilo, watatamani, wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na wakampinga Mtume wasimtii, lau Mwenyezi Mungu Angaliwafanya sawasawa, wao na ardhi, wakawa mchanga ili wasifufuliwe. Na wao hawawezi kumficha Mwenyezi Mungu chochote kilichoko ndani ya nafsi zao, kwa kuwa Mwenyezi Mungu Atakuwa Amefunga midomo yao na kutolewa ushahidi juu yao na viungo vyao wenyewe kwa yale waliokuwa wakiyafanya.