Puis, s’ils te traitent de menteur, alors dis : “Votre Seigneur est Détenteur d’une immense miséricorde mais Sa rigueur ne saurait être détournée des gens criminels.”
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Na wakikufanya mrongo, ewe Mtume, wanaokwenda kinyume na wewe miongoni mwa washirikina, Mayahudi na wengineo, waambie, «Mola wenu, Aliyetukuka na kuwa juu, ni Mwenye rehema kunjufu. Na wala haiyepushwi adhabu Yake kwa watu walitenda maovu wakapata madhambi na wakajitokeza wazi na ubaya. Katika haya pana onyo kwao, kwa kwenda kwao kinyume na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.