Qu’ont-ils donc pour qu’Allah ne les châtie pas, alors qu’ils repoussent (les croyants) de la Mosquée Sacrée, quoiqu’ils n’en soient pas les gardiens, car ses gardiens ne sont que les pieux. Mais la plupart d’entre eux ne le savent pas.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Na vipi wao wasistahili adhabu ya Mwenyezi Mungu na hali wao wanawazuia mawalii wake Waumini kutufu Alkaba na kuswali ndani ya msikiti wa H(arām. Na wao hawakuwa ni mawalii wa Mwenyezi Mungu. Mawalii Wake si wengine isipokuwa wale wanaomuogopa Yeye kwa kutekeleza faradhi Alizoziweka na kujiepusha na mambo ya kumuasi. Lakini wengi zaidi wa makafiri hawajui, na kwa hivyo walidai kwamba wana jambo ambalo wasiokuwa wao wana haki nalo zaidi.