Et ne semez pas la corruption sur la Terre après qu’elle ait été réformée. Et invoquez-Le avec crainte et espoir, certes la miséricorde d’Allah est proche des bienfaisants.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Wala msilete katika ardhi aina yoyote ya uharibifu, baada ya Mwenyezi Mungu kuitengeneza kwa kutuma Mitume, amani iwashukie, na kuimarika kwa utiifu wa Mwenyezi Mungu. Na muombeni Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, mkimtakasia maombi yenu, kwa kuogopa mateso Yake na kuwa na matumaini kupata malipo Yake mazuri. Hakika rehema ya Mwenyezi Mungu iko karibu na wenye kufanya wema.