Que ne t’abuse point la versatilité [pour la prospérité] dans le pays, de ceux qui sont infidèles.1
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Usihadaike, ewe Mtume, kwa yale waliyonayo wenye kumkufuru Mwenyezi Mungu, ya ukunjufu wa riziki, hali nzuri ya maisha na kuhama kwao kutoka mahali kwenda pengine kwa ajili ya biashara na kutaka faida na mali. Kwa muda mchache, yote hayo yatawaondokea na watakuwa ni wenye kufungika na kuwekwa dhamana kwa vitendo vyao viovu.