Et lorsqu’une sourate est révélée, il en est parmi eux qui dit: “Quel est celui d’entre vous dont elle fait croître la foi ? ” Quant aux croyants, elle fait certes croître leur foi, et ils s’en réjouissent.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Na pindi Mwenyezi Mungu Aiteremshapo sura, miongoni mwa sura za Qur’ani, kwa Mtume Wake, basi kati ya hawa wanafiki kuna wanaosema, kwa kukanusha na kufanya shere, «Ni nani wenu ambaye sura hii ilimfanya imani yake, kwa Mwenyezi Mungu na aya Zake, iongezeke? Basi wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake,, kule kuteremka sura, kuliwaongezea waolmani kwa kuijua na kuizingatia na kuiamini na kuitumia, na hali wao wanafurahia Imani na yakini Alizowapa Mwenyezi Mungu.