Voilà donc leurs maisons désertes à cause de leurs méfaits. C’est bien là un signe pour des gens qui savent.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Hayo ni makazi yao, yako matupu, hakuna yoyote ndani yake. Mwenyezi Mungu Amewaangamiza kwa sababu ya wao kuzidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na kumkanusha Nabii wao. Kwa kweli, katika uvunjaji huo na uangamizaji pana mawaidha kwa watu wanaokijua kile tulichowafanya. Na huu ndio mwendo wetu kwa wenye kuwakanusha Mitume.