En effet, Nous avons auparavant fait une recommandation à Adam mais il oublia; et Nous n’avons pas trouvé chez lui de résolution ferme.
Tafsirs
Niveaux
Leçons
Réflexions
Réponses
Qiraat
Hadith
Na kwa hakika tulimuusia Ādam kabla hajakula kutoka kwenye ule mti, asile kutoka kwenye mti huo na tukamwambia kwamba Iblisi ni adui yako na mke wako, basi wasiwatoe nyinyi wawili kutoka Peponi, mkajasumbuka wewe na mke wako duniani. Basi Shetani akamshawishi, naye akamtii na akausahau wasia. Na hatukumpata na nia ya nguvu yenye kumfanya aitunze ile amri aliyopewa.