Pada hari itu mereka semuanya dibangkitkan Allah, lalu diberitakan-Nya kepada mereka apa yang telah mereka kerjakan. Allah menghitungnya (semua amal perbuatan itu), meskipun mereka telah melupakannya. Dan Allah Maha Menyaksikan segala sesuatu.
Tafsir
Lapisan
Pelajaran
Refleksi
Jawaban
Qiraat
Hadits
Na kumbuka, ewe Mtume, Siku ya Kiyama, Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atawahuisha wafu wote na Atawakusanya wa mwanzo na wa mwisho katika uwanja mmoja, Awape habari ya yale waliyoyafanya ya kheri na shari. Mwenyezi Mungu Ameyadhibiti hayo na Ameyaandika katika Ubao Uliohifadhiwa, na Amewatunzia wao katika kurasa za matendo yao na hali wao wameyasahau. Na Mwenyezi Mungu ni Shahidi wa kila jambo, hakuna chochote kinachofichamana Kwake.