Begitulah, bagi setiap nabi, telah Kami adakan musuh dari orang-orang yang berdosa. Tetapi cukuplah Tuhanmu menjadi pemberi petunjuk dan penolong.
Tafsir
Lapisan
Pelajaran
Refleksi
Jawaban
Qiraat
Hadits
Na kama tulivyokufanya, ewe Mtume, uwe na maadui miongoni mwa wahalifu watu wako, tulimfanya kila Nabii, miongoni mwa Manabii, awe na adui kati ya wale wahalifu wa watu wake. Basi vumilia kama walivyovumilia. Na inatosha kuwa Mola wako ni Mwenye kuongoa, ni Mwenye kuilekeza, ni Mwenye kuonyesha njia na ni Mwenye kutoa msaada wa kukusaidia wewe dhidi ya maadui zako.Katika haya pana maliwazo kwa Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye.