Allah menyediakan azab yang keras bagi mereka, maka bertakwalah kepada Allah wahai orang-orang yang mempunyai akal! (Yaitu) orang-orang yang beriman. Sungguh, Allah telah menurunkan peringatan kepadamu,
Tafsir
Lapisan
Pelajaran
Refleksi
Jawaban
Qiraat
Hadits
Mwenyezi Mungu Amewaandalia watu hawa, waliokiuka mipaka na wakaenda kinyume na amri za Mwenyezi Mungu na amri za Mitume Wake, adhabu kali sana. Basi muogopeni Mwenyezi Mungu na mjihadhari na mambo Anayoyachukia, enyi watu wenye akili zilizokomaa, mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo! Kwa hakika Mwenyezi Mungu Ameteremsha kwenu, enyi Waumini, Ukumbusho wa kuwakumbusha nao na kuwazindusha juu ya fungu lenu la kumuamini Mwenyezi Mungu na kuwa watiifu Kwake kivitendo.