En roep naast Allah niet iemand aan waar jullie geen baat bij hebben, noch wat jullie kan kwetsen, maar (in het geval) jullie dat doen, zullen jullie zeker tot de onrechtvaardigen behoren.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Wala usiwaombe, ewe Mtume, wasiokuwa Mwenyezi Mungu miongoni mwa mizimu na masanamu, kwani wao hawanufaishi wala hawadhuru. Na ufanyapo hilo na ukawaomba wasiokuwa Mwenyezi Mungu, hapo wewe utakuwa ni miongoni mwa wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu, wenye kujidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na kufanya maasia. Maneno haya ingawa anaambiwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, pia wanaambiwa umma wote.