En nader de bezittingen van de wees niet, behalve dan om het te vermeerderen, tot hij de leeftijd van de volle wasdom bereikt heeft. En vervul elk verbond. Waarlijk! Over het verbond zal gevraagd worden(op de Dag der Opstanding).
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Wala msitumie mali ya watoto waliofiliwa na wazazi wao nao wako chini ya miaka ya kubaleghe na wakawa wako chini ya usimamizi wenu, isipokuwa kwa njia ambayo ni nzuri kwao, nayo ni kuyazalisha na kuyakuza, mpaka afikie mtoto yatima miaka ya kubaleghe na utumiaji mzuri wa mali. Na timizeni utekelezaji wa kila ahadi mliyojilazimisha nayo, kwani Mwenyezi Mungu Atamuuliza mwenye kuweka ahadi kuhusu hiyo ahadi Siku ya Kiyama, Atamlipa akiitimiza na kuitekeleza na Atamtesa akienda kinyume nayo.