En zij vragen jou om de bestraffing te bespoedigen! En Allah is niet nalatig in Zijn belofte. En waarlijk, één dag met jullie Heer is als duizend jaren in jullie berekening.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Na makafiri wa Kikureshi, kwaujinga wao, wanakuharakisha, ewe Mtme, uwaletee adhabu ambayo uliwaonya nayo baada ya kuwa wakakamavu juu ya ukafiri. Mwenyezi Mungu Hataenda kinyume na ahadi yake ya adhabu aliyowaonya nayo, haina budi kutuka. Na hapa duniani Aliwaharakishia hiyo, siku ya vita vya Badr. Na siku moja miongoni mwa siku mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama miaka alfu moja mnazozihesbu katika miaka duniani.