Denk dus niet dat Allah Zijn belofte aan Zijn Boodschappers niet zou houden. Zeker, Allah is Almachtig, de Bezitter van de Vergelding.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Basi usidhanie, ewe Mtume, kwamba Mwenyezi Mungu Atakwenda kinyume na vile Alivyowaahidi Mitume Wake, kuwa Atawapa ushindi na Atawaangamiza wenye kuwakanusha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mshindi, hakuna kitu kinachomshinda kukifanya, ni Mwenye kuwalipiza maadui wake kwa kuwapa mateso makali kabisa. Maneno haya ingawa anaambiwa Nabii, rehema na amani zimshukie, yanaelekezwa kwa ummah wote.