Maar voor degenen die hun Heer vrezen, zijn er Tuinen waar rivieren onderdoor stromen, zij zijn daarin de eeuwig levenden, een ontvangst van Allah. En datgene wat bij Allah is, is het beste voor degenen die Allah gehoorzamen.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Lakini wale waliomuogopa Mola wao , wakazifuata amri Zake na wakajiepusha na makatazo Yake, Mwenyezi Mungu Amewaandalia mabustani ya Pepo ambayo mito inapita chini ya majumba yake ya fahari na miti yake. Mabustani hayo yatakuwa ni makazi yao ya kudumu; hawatatoka humo. Na yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni makubwa zaidi na bora zaidi kwa watiifu kuliko yale ya starehe za ulimwengu ambazo hao waliokufuru wanatanga huku na kule kwa kuzitafuta.