Maar waarom komen zij voor een besluit naar jou terwijl zij de Thora hebben? Daarin is de Wet van Allah: maar zelfs na dat keren zij zich af. Want zij zijn geen (ware) gelovigen.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Kitendo cha Mayahudi hawa ni cha kushangaza. Wao wanashitakiana kwako, ewe Mtume, na wao hawakuamini wewe wala Kitabu chako, pamoja na kuwa ile Taurati wanayoiamini wanayo, na humo muna hukumu ya Mwenyezi Mungu; kisha wanaondoka baada ya kutoa hukumu yako, iwapo haikuwaridhisha, wakakusanya kati ya kuzikataa sheria zao na kuipa mgongo hukumu yako. Na hawakuwa hao, wanaosifika na sifa hizo, ni wenye kumuamini Mwenyezi Mungu, kukuamini wewe na kuikubali hukumu uliyoitoa.