Waarlijk, Allah! Hij is mijn Heer en jullie Heer. Aanbidt dus alleen Hem. Dit is het (enige) rechte Pad.”
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
«Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ndiye Mola wangu na Mola wenu nyote, basi muabuduni Yeye Peke Yake na msimshirikishe na Yeye kitu chochote. Hili nililowaamrisha la kumcha Mwenyezi Mungu na kumpwekesha kwa ustahiki wa kuabudiwa ndio njia iliolingana sawa, nayo ni Dini ya Mwenyezi Mungu ya kweli Ambaye Hakubali kutoka kwa yoyote dini isiyokuwa hiyo.”