En (gedenkt) toen Wij jullie van de mensen van de Farao redden, die jullie vreselijke martelingen oplegden, jullie zonen vermoorden en jullie vrouwen spaarden, verlosten, en daarin was een machtig vonnis van jullie Heer.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Kumbukeni neema Yetu juu yenu, tulipowaokoa nyinyi na mateso ya Fir'awn na wafuasi wake, waliokuwa wakiwaonjesha nyinyi adhabu kali sana, wakiwaua watoto wenu wa kiume kwa wingi na kuwaacha wanawake wenu kwa kutumika na kudhalilishwa. Katika hilo, ni mtihani kwenu kutoka kwa Mola wenu. Na katika kuokolewa kwenu na yeye, ni neema kubwa ambayo inapasa kwenu mumshukuru Mwenyezi Mungu Aliyetukuka katika kila zama zenu na vizazi vyenu.