Waarlijk! Dit is een Vermaning, wie het dan wil, zal het Pad naar zijn Heer nemen.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Hakika ndani ya sura hii, kwa yaliyomo ya kuvutia na kuogopesha, ya kuahidi mema na kuonya mabaya, kuna mawaidha kwa viumbe wote. Basi mwenye kujitakia wema nafsi yake ya duniani na Akhera, na ashike njia ya Imani na uchamungu itakayomfikisha kwenye msamaha wa Mwenyezi Mungu na radhi Zake.