Dus toen (de gezant met het geschenk) bij Soeleiman kwam, zei hij: “Schenk jij mij rijkdommen? Wat Allah mij heeft gegeven is beter dan wat Hij jullie heeft gegeven! Nee, jullie verheugen je over jullie geschenk.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Mjumbe wa malkia alipokuja na tunu kwa Sulaymān, alisema Sulaymān, akilikataa hilo na akizungumzia neema za Mwenyezi Mungu juu yake, «Mnanipatia mali ili kuniridhisha? Yale aliyonipa Mwenyezi Mungu ya unabii, ufalme na mali mengi ni mazuri zaidi na ni bora zaidi kuliko hayo Aliyowapa nyinyi, bali nyinyi ndio mnaofurahia tunu mnayotunukiwa, kwa kuwa nyinyi ni watu wa kuonyeshana kwa kujifahiri na dunia na kuipapia kwa wingi.»