Als er daarin goden naast Allah zouden zijn geweest, dan waarlijk, beiden (de hemelen en de aarde) zouden vernietigd zijn. Verheerlijkt is Allah, de Heer van de Troon, boven alles wat zij aan Hem toewijzen!
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Lau mbinguni na ardhini kulikuwa na waungu wasiokuwa Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, wenye kuyaendesha mambo yake, ungaliharibika mpango wake. Basi Mwenyezi Mungu, Bwana wa 'Arsh, Ameepukakana na sifa za upungufu na Ametakasika na kila sifa ambayo wakanushaji makafiri wanamsifu nayo ya urongo, uzushi na kila aibu.