En tot Zijn Tekenen behoort jullie slaap ‘s nachts, en jullie zoektocht naar Zijn overvloed overdag. Waarlijk, hierin zijn zeker Tekenen voor mensen die luisteren.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Na miongoni mwa dalili za uweza huu ni kuwa Mwenyezi Mungu Amewawekea usingizi uwe ni mapumziko kwenu ya usiku au mchana, kwani katika kulala yanapatikana mapumziko na kuondokewa na machovu, na Amewawekea mchana ambapo ndani yake mnaenda huku na kule kutafuta riziki. Hakika katika hayo kuna dalili ya ukamilifu wa uweza wa Mwenyezi Mungu na upitishaji matakwa Yake kwa watu wanaosikia mawaidha usikiaji wa kutia akilini, kufikiria na kuzingatia.