Hebben zij niet gezien dat Wij een veilig Heiligdom hebben gemaakt, terwijl de mensen om hen heen worden verdreven? Geloven zij in de leugen en ontkennen zij de gunsten van Allah?
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Kwani hawakushuhudia makafiri wa Makkah kwamba Mwenyezi Mungu Amewawekea Makkah kuwa ni mahali patakatifu penye amani, watu wake wanapata amani humo ya nafsi zao na mali zao, hali watu walio pambizoni mwake, nje ya eneo takatifu, wananyakuliwa hawana amani? Je, ni ushirikina wanaouamini na ni neema ya Mwenyezi Mungu Aliyowahusu wao nayo, wanayoikanusha, wakawa hawamuabudu Yeye, Peke Yake, bila mwingine?