Als jullie een breuk tussen hen beiden vrezen, wijs dan bemiddelaars aan, één van zijn familie en de andere van haar familie; als zij beiden vrede wensen, Allah zal hun verzoening verzorgen. Waarlijk, Allah is voor altijd Alwetend, Kennend.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Na mkijua, enyi wasimamizi wa mume na mke, kuwa kuna ugomvi baina yao unaopelekea kutengana, wapelekeeni mwamuzi muadilifu wa upande wa mume na mwamuzi muadilifu wa upande wa mke, ili watazame na kutoa uamuzi wenye maslahi ya wao wawili. Na kwa kuwa wale waamuzi wawili wana hamu ya kupatanisha na wanatumia njia nzuri, Mwenyezi Mungu Atawatilia taufiki baina ya mume na mke. Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, hakuna chochote kinachofichamana Kwake kuhusu mambo ya waja Wake, ni Mtambuzi wa yaliyomo ndani ya nafsi zao.