Als jullie niet uitrukken, zal Hij jullie een pijnlijke bestraffing geven en jullie door een ander volk vervangen en jullie kunnen Hem in het geheel niet kwetsen. En Allah is tot alle dingen in staat.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Iwapo hamtatoka, enyi Waumini, kwenda kupigana na adui yenu , Mwenyezi Mungu Atawateremshia mateso Yake na atawaleta watu wengine ambao watatoka kwenda vitani waambiwapo watoke, watamtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na nyinyi hamtamdhuru Mwenyezi Mungu chochote kwa kuikimbia kwenu jihadi, kwani Yeye ni mwenye kujitosheleza na nyinyi, na nyinyi ndio wahitaji Wake. Na Analolitaka Mwenyezi Mungu litakuwa hapana budi. Na Mwenyezi Mungu, juu ya kila kitu, ni Muweza, miongoni mwa kutetea dini Yake na Mtume Wake pasi na nyinyi.