En voorwaar, Wij hebben de generaties vόόr jullie vernietigd toen zij onrecht pleegden, terwijl hun Boodschappers met duidelijke bewijzen tot hen kwamen, maar zij behoorden niet tot degenen die geloofden. Zo vergelden Wij het boosaardige volk.
Tafseers
Lagen
Lessen
Reflecties
Antwoorden
Qiraat
Hadith
Hakika tuliwaangamiza watu waliowakanusha Mitume wa Mwenyezi Mungu kabla yenu, enyi mliomshirikisha Mola wenu, waliposhirikisha na wakawajia Mitume wao kutoka kwa Mwenyezi Mungu wakiwa na miujiza iliyo wazi na hoja zenye kubainisha ukweli wa yale aliyekuja nayo. Basi watu hawa hawakuwa ni wenye kuwaamini Mitume wao na kuwafuata, kwa hivyo walistahili maangamivu. Na mfano wa maangamivu hayo ndivyo atakavyolipwa kila mhalifu mwenyekukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu.