Ó fiéis, se vos casardes com as fiéis e as repudiardes, antes de haverde-las tocado, não lhes exigias o cumprimento dotérmino estabelecido; dai-lhes um presente, outrossim, e libertai-as decorosamente.
Tafsirs
Camadas
Lições
Reflexões
Respostas
Qiraat
Hadith
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, mfungapo ndoa na wanawake na msiwaingilie, kisha mkawaacha kabla hamjawaingilia, basi hawalazimiki wakae eda lenu la nyinyi kuwahesabia, basi wapeni kitu cha kuwastarehesha katika mali yenu kulingana na ukunjufu mlionao ili kuwapa maliwazo, na wafungueni washike njia waende zao pamoja na sitara nzuri, bila ya udhia wala madhara.