Eis que os incrédulos malversam as suas riquezas, para desviarem (os fiéis) da senda de Deus. Porém, malversá-las-ãocompletamente, e isso será a causa da sua atribulação; então, será vencidos. Os incrédulos serão congregados no inferno.
Tafsirs
Camadas
Lições
Reflexões
Respostas
Qiraat
Hadith
Hakika ya wale wenye kukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu na wakamuasi Mtume Wake wanatoa mali yao kuwapa washirikina na watu wa upotevu wanaofanana na wao ili kuzuia njia ya Mwenyezi Mungu isifuatwe na kuwazuia Waumini wasimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Basi watatoa mali yao kwa lengo hilo, kisha mwisho wa utoaji wao utakuwa ni majuto na hasara juu yao, kwani mali yao yatamalizika na hawatapata wanaoyatarajia ya kuzima nuru ya Mwenyezi Mungu na kuzuia njia Yake isifuatwe, kisha mwishowe Waumini watawashinda. Na wale waliokufuru watakusanywa wapelekwe kwenye Jahanamu waadhibiwe humo.